Ouattara ateuliwa tena kugombea urais
22 Juni 2025Siku mbili baada ya vyama viwili vikuu vya upinzani nchini humo kutangaza "msimamo wa pamoja" wa kutaka viongozi wao, waliopigwa marufuku katika uchaguzi wa urais wa Oktoba, waruhusiwe kugombea.
Viongozi hao ni rais wa zamani Laurent Gbagbo- wa chama cha PPA-CI na mwenzake Tidjane Thiam's aliyekuwa mfanyakazi wa zamani katika benki za kimataifa wa chama cha PDCI.
Hata hivyo Rais Ouattara mwenyewe bado hajathibitisha iwapo atawania muhula wa nne wa urais wa nchi hiyo ya Afrika magharibi, lakini wajumbewa chama chake waliunga mkono uteuzi wake baada ya mjumbe Patrick Achi, ambaye ni kiongozi wa chama kinachotawala cha RHDP, kumpendekeza.
Mvutano wa kisiasa umekuwa ukiongezeka nchini Ivory Coast tangu mahakama ilipowakataza viongozi kadhaa wa upinzani akiwemo Gbagbo kushiriki katika uchaguzi wa Oktoba 25.