Ocalan aitaka PKK kuweka chini silaha
28 Februari 2025Chama cha PKK kilianza mapambano yake dhidi ya Uturuki tangu mwaka 1984, kwa lengo la kuanzisha dola lao kusini mashariki mwa nchi hiyo.
Mzozo kati ya wapiganaji wa PKK na serikali ya Uturuki ulikuja kuvuuka mipaka na kuingia hadi Syria na Iraq na umesababisha vifo vya maelfu ya watu.
Soma zaidi: Ocalan ataka chama chake cha PKK kuacha mapigano Uturuki
Ocalan, aliyekuja kukamatwa mwaka 1999 akiwa nchini Kenya baada ya kufukuzwa Syria mwaka 1998, amekuwa akitumikia kifungo cha maisha katika kisiwa cha Imrali tangu wakati huo.
Ingawa Rais Tayyip Erdogan wa Uturuki hajawahi kuzungumzia moja kwa moja juhudi za mapatano na kiongozi huyo wa Wakurdi, lakini mnamo mwezi Oktoba mmoja wa washirika wake alisema Ocalan angeliachiwa huru ikiwa angelikubali kukivunja chama chake na kuweka silaha chini.