JamiiMisri
Nchi za Kiarabu zaidhinisha mpango wa kuijenga upya Gaza
5 Machi 2025Matangazo
Mpango huo uliowasilishwa katika kikao chao mjini Cairo, unachukuliwa kama mbadala wa pendekezo lililokosolewa vikali la Rais wa Marekani Donald Trump la kuchukua udhibiti wa Gaza na kuwahamisha Wapalestina, wazo linaloungwa mkono na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu.
Hata hivyo, matarajio ya Mamlaka ya Palestina kuiongoza Gaza baada ya mzozo huo bado ni hafifu hasa ikizingatiwa kuwa Israel inapinga wazo la kuipatia mamlaka hiyo jukumu lolote la uongozi.