Nchi kadhaa za Ulaya zakabiliana na mioto ya nyika
9 Agosti 2025Matangazo
Msemaji wa idara ya zima moto amesema zaidi ya wazimamoto 260 wakiwa na karibu magari 80 ya zima moto na ndege 12 walitumwa karibu na mji wa Keratea, eneo la mashambani lililo umbali wa kilomita 43 kusini mashariki mwa Athens.
Dimitris Loukas, meya wa mji jirani wa Lavrio, amesema moto huo uliozuka Ijumaa umeharibu karibu ekari 10,000 za misitu. Nchi kadhaa za Ulaya ikiwa ni pamoja na Italia na Ufaransa zinapambana na moto wa nyika hasa kutokana na hali ya joto kali linaloshuhudiwa maeneo hayo.