Naibu wa mkuu wa polisi Kenya apisha uchunguzi
16 Juni 2025Matangazo
Makamu wa mkuu wa jeshi la polisi nchiniKenya, Eliud Lagat, anayeandamwa na tuhuma za kuhusika katika mauaji ya mwanablogu, Albert Ojwang, amejiondowa kwa muda kwenye nafasi yake kupisha uchunguzi kuhusu kifo cha mwanablogu huyo.
Ojwang alikufa akiwa chini ya kizuizi cha polisi mjini Nairobi. Katika taarifa yake Lagat, amesema anajiondowa kwenye nafasi yake kama makamu kiongozi wa jeshi la polisi, kutowa nafasi ya kumalizika uchunguzi.
Kadhia ya kifo cha mwanablogu na mwalimu, Albert Ojwang, aliyekuwa na umri wa miaka 31, aliyedaiwa kuikosoa polisi kabla ya kukamatwa kwake, iliibuwa maandamano makubwa mjini Nairobi wiki iliyopita.