Myanmar: waliofariki katika tetemeko la ardhi wafikia 3,300
5 Aprili 2025Matangazo
Fletcher amekutana leo na wahanga wa tetemeko hilo la ardhi katika mji wa Mandalay ulio karibu na kitovu cha mkasa huo ambao kwa sasa unakabiliana na uharibifu mkubwa.
Katika chapisho kwenye mtandao wa kijamii wa X, Fletcher amesema uharibifu huo ni mkubwa na kuongeza kuwa ulimwengu lazima uwasaidie watu wa Myanmar.
Idadi ya vifo baada ya tetemeko la ardhi Myanmar yaongezeka
Kwa kawaida Marekani imekuwa mstari wa mbele katika misaada ya majanga ya kimataifa, lakini Rais Donald Trump amelisambaratisha shirika la misaada ya kibinadamu nchini humo.
Hapo jana, nchi hiyo ilisema kuwa inaongeza dola milioni 7 zaidi kwa msaada wa awali wa dola milioni 2 kwa Myanmar.