Sheria na HakiKimataifa
Mwendesha Mashtaka wa ICC kukaa pembeni kupisha uchunguzi
16 Mei 2025Matangazo
Taarifa hiyo imetolewa hii leo na Mahakama ya ICC yenye makao yake makuu mjini The Hague, Uholanzi.
Mwezi Mei mwaka uliopita Khan alituhumiwa kuwa alijaribu kwa zaidi ya mwaka mmoja kumlazimisha msaidizi wake wa kike kuwa na mahusiano naye ya kimapenzi ikiwa ni pamoja na shutuma za kumpapasa bila ridhaa yake.
Shutuma hizo zilitolewa na wafanyakazi wawili wa mahakama ya ICC waliosema wamesimuliwa na mwanamke anayedai kufanyiwa vitendo hivyo. Khan amekanusha vikali madai hayo dhidi yake.
Tuhuma hizo zilitolewa wiki chache kabla Khan hajawasilisha maombi ya hati za kukamatwa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, waziri wake wa Ulinzi na viongozi watatu wa kundi la Hamas kuhusiana na tuhuma za uhalifu wa kivita ndani ya Ukanda wa Gaza.