SiasaUganda
Mwanaharakati wa Uganda aliyetekwa afikishwa Mahakamani
6 Mei 2025Matangazo
Eddie Mutwe, ambaye jina lake halisi ni Edward Ssebuufu, alikuwa mlinzi wa kiongozi wa upinzani Bobi Wine alikamatwa Aprili 27 na watu wenye silaha karibu na mji mkuu Kampala.
Wakili wa Mutwe, Magellan Kazibwe alisema mteja wake alifikishwa katika mahakama ya hakimu mkuu mjini Masaka takriban kilometa 140 kusini mwa mji mkuu wa Kampala.
Soma pia: Jenerali Muhoozi athibitisha kumshikilia mlinzi wa Bobi Wine
Wiki iliyopita, mtoto wa rais Yoweri Museveni na Mkuu wa Majeshi wa Uganda Muhoozi Kainerugaba, alichapisha kwenye mtandao wa X kwamba alimnasa "kama panzi" mwanaharakati huyo na kwamba alikuwa akimshikilia nyumbani kwake.