Mwanaharakati Boniface Mwangi akamatwa mjini Nairobi
20 Julai 2025Bi Mwangi aliandika katika mtandao wake wa X kwamba polisi waliingia nyumbani kwake na kumkamatwa mumewe kwa madai ya ugaidi. Amesema wamechukua vifaa vyake vya kieletroniki na kumpeleka katika idara ya upelelezi nchini Kenya, DCI.
Taarifa za kukamatwa kwake tayari zimezua hasira miongoni mwa wakenya katika mitandao ya kijamii, huku wengi wakitaka mwanaharakati huyo kuachiwa huru mara moja.
Wanaharakati wa Kenya bado wanazuiliwa Tanzania
Hussein Khalid, Mkurugenzi wa shirika la kutetea haki za binaadamu la Vocal Africa, amethibitisha kukamatwa kwa Boniface Mwangi. Amesema anafuatilia kujua sababu hasa ya kukamatwa kwake.
Mwanaharakati huyo mashuhuri amekuwa akikamatwa mara kadhaa ikiwemo mwezi Mei alipokamatwa alipokuwa Tanzania na kudaiwa kuteswa kwa siku kadhaa na maafisa wa usalama wa taifa hilo jirani.