Mwanadiplomasia mkuu wa Marekania awasili Saudia
17 Februari 2025Matangazo
Mwanadiplomasia huyo mkuu wa Marekani anatarajiwa kujadili na maafisa wa Saudia mapendekezo ya Trump ya kuwahamisha Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza na Washington kuichukua ardhi hiyo.
Soma pia:Ziara ya Rubio: Netanyahu asifu msimamo wa Trump kuhusu Gaza
Rubio amewasili mjini Riyadh akitokea Israel alikoanzia ziara yake jana Jumapili ambako alisisitiza kwamba kundi la Hamas linalotawala Ukanda wa Gaza ni lazima liangamizwe.
"Ni dhahiri Hamas haiwezi kuendelea kuwa kundi la kijeshi au linalotawala serikali. Na kusema kweli kadri linavyobakia kuwa kundi linaloweza kutawala, au linaloweza kuwa kitisho kwa kutumia nguvu, amani haitopatikana. Ni lazima litokomezwe"
Baada ya Saudi Arabia, Rubio ataelekea Umoja wa Falme za Kiarabu.