SiasaAsia
Korea kaskazini yarusha makombora kuelekea Korea Kusini
10 Machi 2025Matangazo
Taarifa hiyo imeongeza kwamba makombora hayo ya Korea kaskazini yalianguka katika mji mmoja kwenye mkoa wa Hwanghae uliopo katika upande wa magharibi wa bahari ya manjano.
Wiki iliyopita, Korea Kaskazini iliituhumu Marekani kwa "uchokozi wa kisiasa na kijeshi" baada ya meli ya Marekani iliyobeba vifaa vya kijeshi kufika katika mji wa bandari wa Busan wa Korea Kusini.
Soma pia:Korea Kaskazini yaishtumu Marekani kwa ''uchokozi''
Marekani hupeleka maelfu ya wanajeshi wake nchini Korea Kusini mara kwa mara kufanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi, ambayo wanayaelezea kuwa ni ya kujihami.