M23 yasitisha mapigano kupisha misaada ya kiutu
4 Februari 2025Matangazo
Muungano wa makundi ya waasi ulioukamata mji huo wa kimkakati umetangaza kusitisha mapigano kwenye eneo hilo ili kupisha huduma za kiutu.
M23 watangaza kusitisha mapigano kupisha misaada ya kiutu
Kusitishwa kwa mapigano kati ya waasi hao na jeshi la Kongo kunatangazwa wakati maelfu ya watu tayari wameyakimbia makazi yao, huku kukitolewa miito ya njia salama za kupitisha misaada.
Muungano huo wa Mto Kongo, unalijumuisha kundi hilo la M23 linaloungwa mkono na Rwanda, waliodaiwa pia kudhibiti maeneo mengine mashariki mwa Kongo, na kusonga mbele kuelekea mji mkuu wa jimbo la Kivu Kusini, Bukavu.