MigogoroSudan
Sudan:Muungano wa RSF watangaza uundwaji wa serikali pinzani
27 Julai 2025Matangazo
Serikali hiyo pinzani iliyotangazwa magharibi mwa Sudan haitozingatia misingi ya kidini na imegawanywa katika mikoa minane na itaongozwa na Jenerali wa kundi la RSF Mohamed Hamdan Dagalo maarufu kama Hemedti.
Hatua hiyo ilipingwa vikali na jeshi la nchi hiyo na inatishia kuigawanya zaidi Sudan inayoshuhudia kwa miaka miwili sasa vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Jeshi la Sudan likiongozwa na Jenerali Abdel Fattah al-Burhan limelaani hatua hiyo na kuahidi kuendeleza mapambano hadi litakapodhibiti eneo zima la Sudan inayokabiliwa na migogoro, mapinduzi, umaskini na njaa.