Mtu mwenye silaha auwa wanne New York
29 Julai 2025Matangazo
Kwa mujibu wa chanzo kimoja cha polisi, mtuhumiwa wa mauaji hayo alikufa baada ya kujipiga risasi mwenyewe.
Meya wa jiji hilo, Eric Adams, aliandika kupitia mtandao wa X kwamba afisa wa polisi alikufa baada ya kupigwa risasi na mshambuliaji huyo.
Majina ya wahanga wengine wa mauaji hayo hawajatajwa, lakini eneo yalikofanyika ni makao makuu ya mashirika makubwa ya kibiashara, yakiwemo ya Colgate Palmolive na KPMG.
Matukio ya mashambulizi ya ovyo ovyo ni jambo la kawaida nchini Marekani, ambako sheria inaruhusu watu kuwa na kutembea na silaha wapendavyo.