Mmoja auawa katika mashambulizi mapya ya Urusi, Ukraine
29 Mei 2025Matangazo
Serikali imesema majengo kadhaa yaliharibiwa pamoja na miundo mbinu katika shambulio hilo lililomjeruhi mwanamke mmoja.
Watu wengine watatu walijeruhiwa katika shambulizi la droni kwenye eneo la viwanda la Dnipropetrovsk. Kulingana na gavana wa jimbo hilo Serhiy Lysak, majengo ya wakaazi yaliharibiwa na paneli 30 za kuzalisha nishati pia ziliharibiwa.
Kwa upande mwengine Urusi nayo imeripoti kudungua droni 48 za Ukraine zilizorushwa mjini Moscow.
Urusi yapendekeza mazungumzo mapya na Ukraine
Barabara ya kuelekea uwanja wa ndege wa Vnukovo mjini humo ilifungwa kwa muda kufuatia shambulio hilo. Urusi na Ukraine zimekuwa katika mgogoro tangu Mowcow ilipoivamia kijeshi Kyiv tarehe 24 mwezi Februari mwaka 2022.